Xpeed imejengwa kwa teknolojia ya kisasa (Flutter & Laravel) ili kuhakikisha kasi, usalama, na urahisi kwa watumiaji wote.
Mfumo wa kipekee kwa Bodaboda. Nunua tokens za 100 Tsh kufanya kazi. Hakuna makato ya asilimia (Commission) au madeni ya wiki.
Ramani yetu imeundwa kutambua vichochoro na maduka ya mtaani ambayo Google Maps haioni. Tunakuunganisha na Duka la Mangi halisi.
Kabla Rider hajaondoka dukani, lazima apige picha mzigo kupitia App. Mteja anaona picha hiyo papo hapo kwa usalama zaidi.
App nzima imetengenezwa kwa Kiswahili fasaha. Maneno rahisi kama "Oda", "Lipa", na "Mteja" yanamfanya yeyote aweze kutumia.
Algorithm yetu inatafuta Rider aliye karibu zaidi (ndani ya 2km) ili kuhakikisha mzigo wako unafika ndani ya dakika 15.
Taarifa zako ni siri. Tunatumia teknolojia ya usalama ya hali ya juu (Encryption) kulinda namba zako za simu na miamala.